Utajiri: Suti Zamtajirisha Bilionea Delano

Utajiri: Suti Zamtajirisha Bilionea Delano


Ukweli ni kwamba, utajiri si bahati. Ni matokeo ya juhudi zako. Ni matokeo ya yale unayoyafanya katika kipindi chote.
Huwezi kusema kwamba umeandikiwa bahati, hivyo ukae chumbani, ujifungie na kusema kuwa, utajiri utakuja tu kwa kuwa umeandikiwa. Bilionea Said Salim Bakhresa, asingeweza kuwa tajiri kama tu angesema kwamba, anakubaliana na hali aliyokuwa nayo kipindi hicho na kukaa tu kwa kuamini ungemfuata.
Nigeria ni moja ya nchi zenye mabilionea wengi hapa Afrika.
Nchi hiyo iliyopo Magharibi mwa Afrika imekuwa ikiongoza kwa miaka kadhaa kuwa na mabilionea, vijana wachapakazi ambao wamepambana kutoka kwenye umaskini na mwisho kuwa mabilionea wakubwa.
Miongoni mwa vijana hao ni Sijibomi Ogundele, Igho Sanomi na wengine wengi.
Mbali na mabilionea hao, leo tunakwenda kumtambua bilionea mwingine kijana ambaye anatikisa kwa kipindi kirefu nchini Nigeria. Ni jamaa anayeitwa Ladi Delano, bilionea mwenye umri wa miaka 37 tu
UTAJIR WAKE
Jamaa ana utajiri mkubwa wa dola bilioni moja hivyo ana jambo la kujifunza kutoka kwake.
 MASKINI KAMA WENGINE
Delano anasema kwamba hakuzaliwa kwenye familia ya kitajiri ila anashukuru kwa sababu baba yake alikuwa mfanyabiashara mdogo kwa
hiyo kila siku alikuwa akimwambia kuhusu kufanikiwa.
Hakuwa akipenda biashara, lengo lake kubwa lilikuwa ni kuwa mwanasheria. Lakini baada ya baba yake kumwambia mengi kuhusu biashara na kwamba angefanikiwa zaidi ya kuwa mwanasheria, alibadili mawazo yake na kuwa mfanyabiashara.
Anaendelea Kusema kwamba katika maisha aliyokuwa akiishi, alitamani sana kumiliki laptop (kompyuta mpakato) lakini alishindwa kwani kumwambia baba yake amnunulie ilihali yeye mwenyewe alikuwa akipambana na umaskini, lilikuwa jambo gumu.
AANZA KUUZA SUTI
Delano anasema alianza kufanya biashara kwa kuuza suti nchini Nigeria. Ilikuwa biashara nzuri na ilimlipa sana kwani suti zake nyingi aliwauzia matajiri ambao walimlipa fedha nzuri hivyo kuzikusanya, akaziongezea na alizopewa na baba yake kisha akaenda zake nchini China.
 BIASHARA YA POMBE CHINA
Delano anasema kuna kipindi alimuomba baba yake kwenda China kwani aliamini huko kulikuwa na fedha nyingi na kwa sababu baba yake alitaka kufanikiwa, akamtafutia fedha na kwenda huko. Akiwa China alijitafutia michongo ambayo hakuweka wazi na kuanza kuuza pombe za rejareja nchini humo.
 AANZISHA KAMPUNI
Baada ya kufanikiwa, Delano aliamua kuanzisha kampuni yake nchini China. Hiyo ilikuwa mwaka 2004, kampuni hiyo iliitwa Salidarnosc Asia, kampuni ambayo inatengeneza pombe iitwayo Solid XS.
Pombe hiyo ilimpa mafanikio makubwa kwani ilikuwa ikiuzwa katika miji ishirini na kwa mwaka alikuwa akikusanya dola milioni 20 (zaidi ya shilingi bilioni 40) kama faida, japokuwa baadaye aliamua kuiuza kwa dola milioni 15 (zaidi ya shilingi bilioni 30).
Delano anasema kwamba baada ya kurudi nchini Nigeria, aliumizwa na hali aliyoikuta kwani asilimia 43 ya vijana walikuwa maskini hivyo aliahidi kuwasaidia kwa kuanzisha kampuni zake na kuwaajiri.
Mwaka 2005 alianzisha Kampuni ya Bakrie Delano ambayo inahusika na madini, gesi, mafuta na kilimo. Mwaka 2012, Delano alitajwa kwenye orodha ya Forbes ya mabilionea wa kufuatiliwa zaidi.
 TUNAJIFUNZA NINI?
Delano anapohojiwa na vyombo vya habari, anasema kilichomfanya kuwa bilionea si bahati bali ni kufanya kazi kwa bidii huku akiendelea kusema kwamba hakuna binadamu asiyefanya makosa.
Kama wewe ukimuoneshea mtu aliyefanikiwa bila kufanya makosa, yeye atakuoneshea mtu asiyefanya makosa na bado hajafanikiwa. Hivyo tupambane na tusiogope kukosea kwenye biashara.

Necta yaitupia mpira Utumishi vyeti feki

SIKU chache baada ya kuwekwa hadharani majina ya watumishi walioghushi vyeti na wenye malalamiko kuanza kumiminika katika ofisi za Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), kutaka ufafanuzi wa uhakiki wa taarifa zao, baraza hilo limewataka watumishi hao kupeleka kwa maandishi malalamiko yao kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Pamoja na Necta kuwataka watumishi hao kwenda kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, walipofika katika ofisi hizo, malalamiko yao hayakupokelewa, kwa kile walichoelezwa kuwa NECTA inapaswa kuwapa taarifa ya nini cha kufanya na hawakuwa na taarifa hiyo bado mpaka jana.

Hata hivyo wakati hayo yakijiri, Waziri katika Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki, alipoulizwa kuhusu suala hilo, alilieleza gazeti hili mjini Dodoma jana kuwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, atalitolea ufafanuzi leo mjini humo.

Hivi karibuni Rais, John Magufuli alikabidhiwa taarifa ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma ambapo watumishi zaidi ya 9,932 walibainika kuwa na vyeti vya kughushi na alitangaza kuwafuta kazi na aliwapa siku 15, wawe wameondoka kazini, la sivyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma, alichapisha sehemu ya kwanza majina ya watumishi hao katika vyombo vya habari na jana baadhi ya watumishi walianza kumiminika katika ofisi za Necta, kutaka kujua kasoro za vyeti vyao.

Katika kushughulikia tatizo hilo, Baraza hilo kupitia kwa Katibu Mtendaji wake, Dk Charles Msonde limewataka watumishi wa umma wenye malalamiko kuhusu matokeo ya uhakiki wa vyeti vyao, wawasilishe malalamiko yao kwa maandishi kwa Katibu Mkuu Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia kwa waajiri wao na barua hizo za malalamiko, ziambatanishwe na nakala za vyeti husika.

Dk Msonde aliliambia HabariLeo kuwa wameamua kutumia njia hiyo, kwa kuwa Katibu Mkuu Utumishi ndie mwajiri na wao hufanya kazi na mwajiri na si mfanyakazi mmoja mmoja. Alisema ni ukweli ulio wazi kuwa watumishi wengi, walifanya ‘uchakachuaji’ katika vyeti vyao, walivyoviwasilisha awali wakati wa kuomba ajira na walipotakiwa kuleta vyeti halisi walibaini kuwa kuna tofauti.

“Kazi tuliyofanya sisi hapa baraza ni kuhakiki vyeti ambavyo tuliletewa na waajiri kuweza kubaini uhalali wake, lakini tuliyoyabaini ni mengi sana, watumishi wamekuwa wanafanya udanganyifu sana katika vyeti vyao,” alisema DkMsonde.

Aidha, kutokana na tangazo hilo, gazeti hili liliamua kufika katika Ofisi za Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na kujionea baadhi ya watumishi wakifika kwa malalamiko, lakini lilipotaka ufafanuzi, lilielezwa kwamba msemaji ni Katibu Mkuu na yupo Dodoma.

Akizungumzia suala hilo, mmoja wa walalamikaji ambae hakutaka jina lake litajwe gazetini, alisema alifika NECTA saa 1 asubuhi na alikutana na walalamikaji wengi na mlinzi aliyekuwepo, aliwauliza nini tatizo na wakasema wanataka sehemu wanapohakiki vyeti.

“Mlinzi alituambia tusubiri saa 2:30 tutahudumiwa, lakini ilipofika saa 2:10 Ofisa mmoja wa NECTA alikuja na akabandika tangazo hilo kwenye ubao, baadae tukaona hamna msaada hapo mimi nikaamua kurudi ofisini nikaandika barua ya malalamiko nikapitisha kwa mwajiri wangu nikaelekea utumishi,” alisema.

Alisema alipofika Utumishi, aliwakuta walalamikaji wengine na baadae wakaenda chumba namba 6A, ambapo walimkuta ofisa mmoja (jina lake limehifadhiwa), akawaambia utaratibu haupo, hivyo kwa kuwa NECTA walipaswa wawasiliane nao kwanza.

“Sisi tulipofika alituambia kwamba Katibu Mkuu Utumishi hajatoa waraka na anatakiwa kwanza atoe maelekezo ili wajue wanayashughulikia vipi matatizo hayo na baadae alituonesha majina aliyokuwa nayo ni yale yaliyotoka kwenye gazeti na baraza ndiyo walipaswa kueleza kwamba yana tatizo gani,” alisema.

Kutokana na hayo, walalamikaji hao walionekana kukerwa na kauli hiyo na kudai kwamba wameonewa, kwa kuwa mtuhumiwa yeyote, lazima apewe muda wa kujitetea lakini wao hawakufanyiwa hivyo.

“Wote sisi tumeona majina gazetini na hatukuitwa kusikilizwa wakati ni haki yetu ya msingi, walipoona kama kuna makosa walipaswa watuite tujitetee lakini wao hawakufanya hivyo.

Sisi tulijitokeza tulitaka tuwe wa kwanza maana kuna wengi wanakuja hadi kutoka mikoani na tunaambiwa mwisho ni Mei 15…Tunaomba suala hili lishughulikiwe kwa haraka,” alisema.

Bungeni mjini Dodoma jana, Waziri anayeshughulikia utumishi wa umma, Kairuki alipoulizwa kuhusu malalmiko hayo, alisema leo Katibu Mkuu Utumishi atatolea ufafanuzi suala hilo.

Hata hivyo, baada ya Rais kupokea majina hayo ya waliobainika kuwa na vyeti feki, aliagiza kusitishwa mara moja mishahara yao, huku akiwataka waondoke kazini mara moja na watakaokaidi agizo hilo, watashitakiwa mahakamani.

Rais Magufuli alisema ni lazima watumishi hao, waondoke kwenye utumishi wa umma mara moja kutokana na kuisababishia serikali hasara kubwa. “Tena naagiza mshahara wao wa mwezi huu ukatwe na waondoke kwenye utumishi wa umma, watakaokaidi watapelekwa mahakamani kwa mujibu wa sheria na nafasi hizo 9,932 zitangazwe ili wasomi waweze kuziomba”.

Aidha, alitaka watumishi 1,538 ambao vyeti vyao vina utata mpaka Mei 15, mwaka huu, hatma yao ijulikane na kama wanajijua kuwa si wahusika wa vyeti hivyo waondoke mapema.

Katika hatua nyingine, Halmashauri ya wilaya ya Lindi mkoani Lindi imeanza kufanya mkakati wa kutafuta watumishi wa afya kwa ajili ya Zahanati za Mkanga II na Shuka kutokana na wahudumu wengi akiwemo dereva wa gari la wagonjwa, kuondolewa kazini mwishoni mwa wiki kutokana na kuwa na vyeti feki.

Hali ya huduma katika zahanati hizo inaelezwa kuwa si nzuri kutokana na kuondolewa kwa watoa huduma hao na tayari halmashauri imesema imenza kuchukua hatua. Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Lindi, Samweli Warioba alithibitisha wakati alipokuwa akizungumza na gazeti hili jana.

Alisema kuna tatizo la wahudumu wa afya kutokana na baadhi kuondolewa wa vyeti feki. Hata hivyo, hakufafanua kama wahudumu hao, atawapata wapi kwa haraka kutokana na zahanati hizo kutegemewa na wakazi wengi wa wilaya hiyo na maeneo ya karibu.

Ofisa wa Afya ambaye hakutaka kutaja jina lake alisema kwamba wakati ambako watumishi hao hawajaondoka, bali kulikuwapo na upungufu wa watumishi wa afya zaidi ya 14, hata kabla ya Rais kutangaza walioghushi na kuondolewa.

Huko bungeni, Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema taasisi hiyo haina mfanyakazi mwenye cheti feki hata mmoja, wafanyakazi wake kwa asilimia 100 wana vyeti halali vya taaluma zao na hiyo inatokana na utendaji bora wa mhimili huo.

Ndugai alisema hayo jana bungeni akizungumzia utendaji wa Bunge. Alisema Bunge ni miongoni mwa taasisi ambazo zina wasomi wengi, na kwamba ukiweka kwenye mizani itakuwa miongoni mwa tatu zenye wasomi wengi nchini.

Spika wa Bunge alitoa sifa hizo, kutokana na uvumi kuenea kwamba Bunge lina wabugne wengi wanaojua kusoma na kuandika tu, akasema ukiweka kwenye uwiano taasisi hiyo ina wasomi wengi mno.

Bunge lenye wafanyakazi 314, ni taasisi mojawapo ambayo ina wasomi wengi kama ukiweka kwenye mizani itakuwa miongoni mwa taasisi tatu za juu zenye wasomi wengi. Alisema hili ni bunge la wasomi, ukichukua maelezo yao hutaona kwamba kuna wabunge wanaojua kusomana kuandika tu, bali ni wasomi.

“Bunge lina wasomi wengi, hata kuzidi baadhi ya vyuo vikuu nchini, hakuna wafanyakazi ambao hawana elimu katika taasisi hiyo mchanganyiko ya wafanyakazi na wabunge,” alisema.

Spika Ndugai aliwapongeza wafanyakazi wa taasisi hiyo walioibuka kuwa wafanyakazi hasa mfanyakazi katika ofisi ya Katibu wa Bunge, Lydia Mpyiana ambaye ni mfanyakazi bora na atazawadiwa Sh milioni 10 kama motisha kwa utendaji wake. Imeandikwa na Mroki Mroki, Hellen Mlacky, Dar, Magnus Mahenge, Dodoma na Kennedy Kisula, Lindi.

VIDEO: NEC Yatangaza Nafasi Iliyoachwa na Mbunge Elly Macha

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza nafasi  ya mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya Chadema
Nafasi hiyo imetangazwa baada ya kifo mbunge aliyekuwa anashikilia wadhifa huo, Dk Elly Macha kufariki dunia Machi 31, mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana  (Jumanne) na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage ni kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemjulisha kuwepo kwa nafasi hiyo.
“Kutokana na kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge wa Viti Maalum, taratibu za kujaza nafasi hiyo zinaendelea kwa kuzingatia Ibara ya 78 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343,”amesema.

MAGUFULI Ageukia 'Waliofoji' Umri..!!!


RAIS John Magufuli amesema serikali inawachunguza watumishi wa umma waliogushi umri ili wasibaki kwenye utumishi wa umma kwa muda ambao hawakustahili kuwa kazini.


Kadhalika, amesema kuna watumishi wenye miaka 60 na zaidi ambao hawataki kustaafu huku waking’ang’ania ajira na madaraka, na wengine wakijipachika vyeo vya ukurugenzi.

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi) ambazo kitaifa zilifanyika jana katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Rais Magufuli alisema uchunguzi huo wa umri umeshaanza.

“Wako watumishi ambao wamebadilisha umri wao," alisema Rais Magufuli. "Wamebadilisha miaka yao na unakuta ni mzee kabisa, lakini kabadilisha umri."
"Kuna watu ambao ni wazee tena kuliko mimi. Wanasema hawaondoki eti ndio wakati umefika, hao nao tunawachunguza.”

Katika hotuba yake, Rais Magufuli alisisitiza kuwa wapo watumishi wa umma ambao bado wanafanya kazi wakiwa wameshatimiza umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 lakini hawataki kustaafu ili kuachia nafasi wegine waajiriwe.

Uchunguzi huo unakuja siku chache baada ya serikali kufanya uhakiki wa vyeti vya elimu vya wafanyakazi wake na kugundua takriban watumishi 10,000 wana vyeti vya kughushi. Wamefukuzwa kazi mara moja.

Akionyesha kukerwa na hali hiyo Rais Magufuli alisema:

“Sheria za nchi yetu hazijasema mtu anayetakiwa kufanya kazi lazima awe na digrii, kila kazi ina qualification (sifa) zake.

"Haiwezekani Watanzania wote wakawa na digrii, darasa la saba wanaajiriwa, form four (kidato cha nne) wanaajiriwa na wenye certificate (cheti) wanaajiriwa.

"Na kila mmoja ana wajibu wa kuajiriwa.

”Tunachosisitiza hapa kama wewe ni darasa la saba na unataka kuajiriwa kaombe kazi ya darasa la saba, kama wewe ni form four kaombe kazi ya form four, kama una certificate nenda ukaombe kazi ya certificate. Usiende ukatafute mavyeti ya kufoji ukajiita daktari kumbe hata unesi haujafikia,”alisema
Aidha, Rais Magufuli alisema wako watumishi ambao wamekuwa wakijiita wakurugenzi, "watu wakubwa wakubwa tu, wana mavyeti ya kufoji, halafu wanawanyanyasa hawa watu wa chini ambao wana vyeti halali."

Alisema kundi hilo nalo ni miongoni mwa watumishi wa umma ambao serikali imekuwa ikiwaamini lakini imegundua kumbe hawastahili nafasi hiyo.

Mbali na kuahidi kushughulikia watumishi walioghushi umri ili kufanya kazi nje ya miaka ya kustaafu, Rais Magufuli alistahili kurejesha nyongeza ya kila mwaka ya mishahara na upadishaji watumishi madaraja.

Download mp3 | Serge_Beynaud_Ft._Diamond_Platnumz_Zimbolo

Download mp3  Serge_Beynaud_Ft._Diamond_Platnumz_Zimbolo

-| Mp3 
Downloadmp3| Serge_Beynaud_Ft._Diamond_Platnumz_-_Zimbolo| Click Download Mp3 Down

Download mp3 |Nikki_Mbishi_-_I'm_Sorry_JK

Download mp3 | Nikki_Mbishi_-_I'm_Sorry_JK| Mp3 
Download mp3 | Nikki_Mbishi_-_I'm_Sorry_JK| Click Download Mp3 Down

Download mp3 | Rundatrax-Africa-ft.-Runtown-Diamond-Teddy

Download mp3 | Rundatrax-Africa-ft.-Runtown-Diamond-Teddy-| Mp3 

Download mp3 | Rundatrax-Africa-ft.-Runtown-Diamond-Teddy| Click Download Mp3 Down




Download mp3 | Navy Kenzo Ft. Patoranking - BAJAJi

Download mp3 | Navy Kenzo Ft. Patoranking - BAJAJi| Mp3
Download mp3 | Navy Kenzo Ft. Patoranking - BAJAJi| Click Download Mp3 Down



Download mp3 | Spicy Ft . Lady Jay Dee – Together

Download mp3 | Spicy Ft . Lady Jay Dee – Together'| Mp3 




Download mp3 | Spicy Ft . Lady Jay Dee – Together| Click Download Mp3 Down


New AUDIO | IYO_-_Loving_You_Ft._Diamond_Platnumz_ | Mp3

DOWNLOAD New AUDIO |IYO_-_Loving_You_Ft._Diamond_Platnumz_| Mp3 

IYO_-_Loving_You_Ft._Diamond_Platnumz_  | Download Mp4 Click Down

IYO_-_Loving_You_Ft._Diamond_Platnumz_
| Download Mp3 Click Down





New AUDIO | DAYNA NYANGE Ft BILL NASS - KOMELA | Mp3

DOWNLOAD New AUDIO | DAYNA NYANGE Ft BILL NASS - KOMELA (New Song 2016) | Mp3 


DAYNA NYANGE Ft BILL NASS - KOMELA (New Song 2016) | Download Mp3 Click Down